Aug 8, 2013

Wanawake waingereza washambuliwa Zanzibar.

Maji ya Acid.
Polisi katika kisiwa cha Zanzibar wamesema wanawake wawili wa Uingereza wamerushiwa maji ya Acid katika nyuso zao baada ya kuvamiwa mwendo wa usiku.

Naibu kamishna wa polisi amesema kuwa wanaume wawili waliwatendea wanawake hao kitendo hicho walipokuwa wakitembea katika barabara za mji wa kihistoria wa zanzibar.

Amesema kuwa polisi tayari wameanzisha msako dhidi yao wanaume hao.

Wanawake hao, wanasemkana kufanyia kazi shirika moja la kujitolea na nia ya shambulizi halo haijulikani.

Chanzo:- BBC

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...